Mabadiliko ya tabianchi hutokea kieneo au hata duniani kote kila baada ya muda fulani. Mabadiliko hayo yanatazamwa moja kwa moja kutokana na vipimo vya angahewa kwa miongo ya miaka au kwa kufanyia utafiti viini vya mashimo yaliyotobolewa kwenye ardhi au barafu ya Aktiki.
Mabadiliko hayo yanaweza kusababishwa na mabadiliko ya kiasi cha nuru ya Jua kinachofika duniani pamoja na mabadiliko katika angahewa ya dunia. Mabadiliko ya tabianchi yaliyojadiliwa sana tangu mwisho wa karne ya 20 yanahusu kuongezeka kwa gesi joto kutokana na shughuli za binadamu, hasa kuchomwa kwa fueli kisukuku.
Mabadiliko hayo yanaweza kusababishwa na mabadiliko ya kiasi cha nuru ya Jua kinachofika duniani pamoja na mabadiliko katika angahewa ya dunia. Mabadiliko ya tabianchi yaliyojadiliwa sana tangu mwisho wa karne ya 20 yanahusu kuongezeka kwa gesi joto kutokana na shughuli za binadamu, hasa kuchomwa kwa fueli kisukuku.